Tajirika na Zao la Soya (Glycine max) - Part 2


....kutokana na mavuno ya soya, mkulima anaweza kupata mapato mengi ukilinganisha na mazao kama mahindi na maharage kwa eneo lililosawa na eneo la soya. Ukweli huu unabainishwa na tathmini iliyofanyika mwaka wa 2005 na Wizara ya Kilimo na Chakula, juu ya hali kilimo cha soya nchini.



4. WADUDU, MAGONJWA NA WANYAMA WAHARIBIFU

Wadudu
Wadudu mafuta (Aphids)
Kwa sasa, nchini Tanzania soya haishambuliwi sana na wadudu kama ilivyo sehemu nyingine ambako zao hilo hulimwa kwa wingi. Hata hivyo endapo wadudu watatokea mkulima anashauriwa kutumia dawa za wadudu kama Thiodan 35% EC na Sumithion 50% EC kwenye kipimo cha mililita 40 za dawa na lita 20 za maji au kipimo kinacho pendekezwa katika dawa husika. Upuliziaji wa dawa ufanywe kulingana na kiasi cha mashambulizi ya wadudu kwenye mazao. Tofauti na mazao kama mahindi na maharage, hakuna wadudu
waharibifu wa soya ghalani. Hivyo zao hilo linaweza kutunzwa kwa muda mrefu ghalani bila kuwa na athari za wadudu. Kwa mkulima na wafanyabiashara, kutokuwepo wadudu waharibifu ghalani kunapunguza gharama za utunzaji hadi bei nzuri itakapofi kiwa.

Mmea wa soya ulioshambuliwa na wadudu mafuta

Magonjwa
Ugonjwa wa blait wa bakteria
Kama ilivyo kwa wadudu, magonjwa ya soya ni machache. Hata hivyo magonjwa ambayo hutokea kwa nadra ni yale yanayotokana na vimelea vya ukungu (fungus) na bakteria. Magonjwa hayo huenezwa kwa mbegu, masalia ya mimea shambani na wadudu mafuta (aphids).
Hivyo ni bora kwa mkulima kuzingatia kanuni za kilimo bora au kupata ushauri wa kitaalamu ili kuepukana na magonjwa hayo. Njia mojawapo ya kuzuia kuenea kwa magonjwa katika zao la soya ni kupanda mbegu safi na zilizopendekezwa mahali husika. Aidha, panda kwa mzunguko (crop rotation) kwa kutumia mazao yasiyoshambuliwa na magonjwa ya soya kama alizeti na mahindi.

Wanyama waharibifu
Kwa kawaida soya hupendwa sana na panya wa shambani na ghalani. Wanyama wengine ni pamoja na sungura, paa, swala, n.k. Mkulima anashauriwa kutumia mbinu na njia mbalimbali zikiwemo za asili, kukabiliana na wanyama hao bila kuharibu mazingira.

Uliikosa Part 1? Soma hapa

5. KUVUNA, KUPURA NA KUHIFADHI SOYA

Kuvuna
Soya tayari kwa kuvunwa
Soya huchukua wastani wa miezi mitatu hadi saba kukomaa kutegemea na aina, mahali ilikopandwa na utunzaji wa shamba. Kwa mfano soya aina ya Bossier huchukua miezi mitatu hadi minne kukomaa na aina ya Uyole Soya 1 miezi minne hadi mitano. Dalili za soya kukomaa ni wakati majani yanapokuwa na rangi ya njano. Anza kuvuna baada ya majani kuanza kupukutika.
Soya ikikauka, maganda yake hupasuka na mbegu hupukutikia chini. Kwa hiyo mkulima anashauriwa kuwahi kuvuna soya mara inapokomaa na kuanza kukauka. Ili kuzuia upotevu wa zao shambani, inashauriwa kuvuna majira ya asubuhi au majira ambayo sio ya jua kali endapo soya imekauka na kuanza kupasuka wakati wa kuvuna.

Kupura/kupiga
Soya haitakiwi kupigwa kwa nguvu kwa sababu mbegu zake hupasuka kirahisi. Mara baada ya kupura, ondoa takataka na uchafu mwingine kwenye soya kwa kupepeta na kupembua. Kausha soya kufi kia wastani wa asilimia 10 ya kiasi cha maji (moisture content) kisha ihifadhi ghalani kwa matumizi au kusubiri soko.

Kuhifadhi
Hifadhi soya baada ya kuhakikisha kuwa imekauka vizuri. Ni muhimu kuhifadhi soya mahali pakavu ili soya isipate uvundo na kuharibu soya ya mbegu na ya chakula. Soya inaweza kuhifadhiwa kwenye vihenge au kwenye magunia kama mazao mengine, tofauti ni kutohitajika dawa ya kuhifadhia.

6. MAVUNO NA MAPATO YATOKANAYO NA ZAO LA SOYA

Mavuno
Soya ina uwezo wa kutoa kilo 1,500 hadi 2,500 kwa hekta kutegemea na aina, hali ya hewa, rutuba ya udongo, matumizi ya mbolea na utunzaji kuanzia wakati wa kuchagua mbegu, kulima, kupanda na kuvuna. Kiasi hicho cha mavuno ni sawa na kilo 600 hadi 1,000 kwa ekari moja.

Mapato
Kutokana na mavuno ya soya, mkulima anaweza kupata mapato mengi ukilinganisha na mazao kama mahindi na maharage kwa eneo lililosawa na eneo la soya. Ukweli huu unabainishwa na tathmini iliyofanyika mwaka wa 2005 na Wizara ya Kilimo na Chakula, juu ya hali kilimo cha soya nchini. Tathmini hiyo ilionyesha kuwa wastani wa gharama za kuzalisha kilo moja ya soya kwa mikoa ya Nyanda za Juu za Kusini hususan Songea Vijijini ni shilingi 130, kwa hiyo kama mkulima atauza soya kwa wastani wa shilingi mia mbili (200) kwa kilo moja bila gharama ya kusafi risha mbali na kijijini kwake anaweza kupata faida ya kati ya shilingi 105,000 hadi 175,000 kwa hekta moja au kati ya shilingi 42,000 na 70,000 kwa ekari moja. Hata hivyo mapato yanaweza kuongezeka endapo mkulima atatunza na kuuza soya wakati bei imepanda kwa kuwa soya inaweza kutunzwa muda mrefu bila kuharibiwa na wadudu. Nidhahiri kuwa zao la soya linaweza kumuongezea mkulima kipato na kumuondolea umaskini.

Soma Tajirika na Zao La Soya - Part 1 

MAREJEO
1. File NAL/S./17/124. (2005). Soybean in Southern regions of Tanzania. Dr. Mponda, O. K. K. ARI Naliendele. Personal communication

2. Laswai, H. S., Kulwa, K. B. M., Ballegu, W. R. W., Silayo, V. C. K., Ishengoma, C. G.; Makindara, J. A.; Mpagalile, J. J. and Rweyemamu, C. L. (2005). Soya kwa lishe bora. Virutubisho na matayarisho yake kwa mapishi mbalimbali. SUA NORAD Focal Programme.

3. Mhagama, G. (2005). Soya: The golden seed in Tanzania. Sunnhemp seed bank. Mruma Centre, Peramiho Songea. Personal communication.

4. Madata, C. (Januari, 2005). Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. ilimo bora cha soya nyanda za juu kusini na Vyakula vya soya na mapishi yake: Soya kwa afya yako. Toleo la Tatu.

Labels: