Kilimo cha zao la vanilla - part 2

Uzalishaji-wa-zao-la-vanilla

Katika kipindi kilichopita tuliona mahitaji ya zao la vanilla na jinsi linavyolimwa, sasa leo napenda kukukaribisha ndugu yangu mkulima katika sehemu hii ya pili ambapo tutaona: magonjwa na wadudu waharibifu wa zao la vanilla likiwa shambani pamoja na kuvuna, kukausha na soko lake. Karibu...


MAGONJWA, WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU

Mmea wa vanilla kwa kawaida haushambuliwi mara kwa mara na magonjwa au wadudu waharibifu kama shamba limetunzwa vizuri. Mashambulizi ya magonjwa na wadudu waharibifu ni dalili ya utunzaji duni wa shamba. 

Ili kuepuka hali hiyo, ni muhimu kukagua shamba kila wakati kubaini na kurekebisha yafuatayo:
Kulisha marando kila mara kunaongeza uwezo wa mizizi kuchukua chakula ardhini hivyo mmea hukua vizuri. Mmea wenye afya nzuri haushambuliwi na magonjwa pia hustamilii mashambulizi ya wadudu waharibifu.

Magonjwa

(i) Kuoza kwa Mizizi (Root rot)

Ugonjwa huu husababishwa na kuvu inayoitwa Fusarium batatis Woollenw.var. vanillae Tucker.

Dalili


Kudhibiti

(ii) Chule ya Majani, Matunda (Anthracnose)

Ugonjwa huu husababishwa na aina ya kuvu inayojulikana kama Calospora vanillae Massee.

Dalili


Kudhibiti

(iii)Ubwiri Vinyoya (Downy mildew)

Husababishwa na kuvu aina ya Phytophthora jatrophae Jens ambao hushambulia mti wa Jatropha unaotumika kama muega. Pia hushambulia mapodo yakiwa shambani na baada ya kuvunwa.

Dalili: Mapodo ya vanilla na majani ya jatropha huwa ukungu mweupe.

Kudhibiti

Wadudu, Ndege na Wanyama Waharibifu

(i) Wadudu

Wadudu wanaoweza kushambulia vanilla ni pamoja na katapila na jongoo.



Kudhibiti: Kagua shamba mara kwa mara ili kutambua kuwepo kwa wadudu hao na kuwaua.



Kudhibiti: Kagua shamba mara kwa mara na kuwaua.

(ii) NdegeKuku

Huharibu mmea kwa kuparura juu ya ardhi na kusababisha kujeruhi na kukata mizizi. Uharibifu huu husababisha mmea kuwa katika mazingira rahisi ya kushambuliwa na vimelea kama Fusarium batatis ambao huozesha mizizi ya mmea.

Kudhibiti: Zuia kuku wasiingie shambani.

(iii) Konokono

Husababisha uharibifu zaidi kipindi cha mvua. Wanapotambaa kwenye mmea huacha utando, hasa katika sehemu inayochipua na kusababisha mmea kudumaa.

Kudhibiti

UVUNAJI

Mapodo ya vanilla hukomaa na kuwa tayari kuvunwa baada ya miezi sita hadi tisa tangu maua kuchavushwa.

Hatua za Kukomaa kwa Vanilla

Ukomaaji wa podo (harage la Vanilla) la vanilla hupitia hatua tano zifuatazo:
  1. Podo hurefuka na kuwa na rangi ya kijani iliyokolea.
  2. Ncha ya podo hubadilika na kuwa njano.
  3. Rangi ya njano husambaa taratibu katika podo.
  4. Ncha ya podo hubadilika rangi na kuwa ya kahawia
  5. Podo hupasuka kuanzia chini.

Jinsi ya kuvuna

Uvunaji wa zao la vanilla huzingatia hatua za ukomaaji wa podo na njia ya ukaushaji itakayotumika. Mapodo huvunwa kwa kukata kikonyo kutumia kisu kidogo.

Vanilla-iliyovunwa


Mavuno

Mavuno ya zao la vanilla hutofautina kulingana na umri wa mmea na utunzaji wa shamba. Mavuno ya kwanza huanza kati ya miaka miwili na nusu hadi mitatu kwa wastani wa kilo moja sawa na mapodo 50 hadi 60. Mmea unapofikia umri wa miaka minne hadi nane, mavuno huongezeka kufikia kilo tatu hadi tano kwa mmea. Hata hivyo mavuno huweza kupungua mmea unapofikia miaka 15 na kuendelea. Hekta moja ya shamba la vanilla lililotunzwa vizuri hutoa mavuno tani tatu hadi tano za mapodo mabichi sawa na wastani wa kilo 500 hadi 800 za mapodo yaliyokaushwa kwa mwaka.

Soma Kilimo cha tangawizi


UKAUSHAJI NA UHIFADHI

Mapodo ya vanilla hukaushwa kwa njia mbalimbali kulingana na utaalamu unaotumika, vifaa vilivyopo na matakwa ya mnunuzi. Ili kupata ubora unaotakiwa, mapodo yakaushwe mara baada ya kuvunwa. Njia za ukaushaji zinazotumika zaidi ni Bourbon na Mexico. Njia hizi huhitaji uangalifu na utaalamu wa kutosha ili kupata madaraja mbalimbali, ladha, na harufu inayohitajika. Njia zote mbili hupitia katika hatua kuu nne za ukaushaji. Hapa nchini, njia ya ukaushaji inayotumika kwa sasa ni Bourbon.

Soma kilimo cha binzari

Ukaushaji kwa Njia ya Bourbon

Njia hii ya ukaushaji huhusisha hatua zifuatazo:

Kuchovya Mapodo kwenye Maji moto (Blanching).

Hatua hii huyazuia mapodo yasiendelee kukomaa na kuanza kutoa ladha.

Kuhifadhi Joto (sweating)

Lengo la hatua hii ni kuongeza joto katika mapodo ili kuruhusu vimengĂ­enya (enzymes) kufanya kazi ya kutoa kemikali ya vanillin ambayo huongeza ladha na harufu inayohitajika.

Kukausha

Katika hatua hii, mapodo huanikwa asubuhi au jioni wakati jua sio kali.

Vanilla-iliyokaushwa


Kuhifadhi Ladha

Hii ni hatua ya mwisho katika mtiririko mzima wa ukaushaji. Katika hatua hii, mapodo huwekwa katika makasha maalumu kwa muda wa miezi mitatu hadi mitano ili kuongeza ladha ya vanilla.

Soma hapa fursa ya kilimo cha mazao ya viungo Morogoro

Kufungasha

Vanilla iliyokwisha kaushwa vizuri hufungashwa kulingana na madaraja. Uzito wa kila kifungu na aina ya ufungashaji hutegemea mahitaji ya soko. 

Zao la vanilla lina thamani kubwa sana sokoni, lakini ni vizuri ufanye utafiti juu ya bei na soko lake kabla hujaanza uzalishaji. Hii itakupa uhakika na matumaini ya kukifanya kilimo hiki kwa moyo zaidi! Kama uliikosa sehemu ya kwanza isome hapa. Comment hapa chini kwa maoni au ushauri juu ya kilimo hiki.

Labels: , ,