Shirika la Wakulima Wetu Tarime (WAWETA) ni shirika lisilokuwa la kiserikali lililo
anzishwa mwaka 2014 na kusajiriwa chini ya sheria ya usajiri mashirika Na. 24
kifungu 12 (2) ya mwaka 2002 na kupata Namba OONGO/08208 likiwa na lengo la
kuwajengea uwezo Wakulima na Wafugaji kwa kutoa elimu ya Kilimo na ufugaji
wenye tija na endelevu.
Kutokana na mikakati ya Shirika ya mwaka 2017, Shirika linahitaji kuajiri nafasi
moja (1) ya MRATIBU wa SHIRIKA ambaye atasimamia shughuli za shirika Wilayani
Tarime kwa kushirikiana na Bodi ya Shirika WAWETA ili kufikia malengo
iliyojipangia.
SIFA ZA MUOMBAJI:
1) Awe Mtanzania mwenye akili timamu,
2) Asiwe na historia ya kushitakiwa kwa makosa ya jinai,
3) Awe na umri kati ya miaka 22 hadi 45,
4) Awe na elimu ya kidato cha IV na kuendelea
5) Awe na cheti cha stashahada (Diploma) ya Kilimo na mifugo kutoka chuo
kinacho tambuliwa na serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, Kama
atakuwa amepata elimu nje ya nchi ni lazima aambatanishe cheti kilicho
thibitishwa na baraza la vyuo na ufundi (NACTE).
6) Awe na uwezo wa kufanya kazi na vikundi vya Wakulima.
7) Awe na leseni ya kuendesha chombo cha moto hususani pikipiki.
JINSI YA KUOMBA
Barua ya maombi iliyoambatanishwa na nakala za vyeti vya elimu, kitambulisho
cha mpiga kura, cheti cha kuzaliwa , na au barua ya uthibitisho kutoka ofisi ya
mtaa au kitongoji, namba ya simu pamoja na barua pepe ya muombaji yatumwe
kwa barua pepe:
waweta.tarime@yahoo.com
AU
Anuani Ifuatayo:
MWENYEKITI
SHIRIKA LA WAKULIMA WETU TARIME (WAWETA)
S.L.P. 16
TARIME
Pia maombi yanaweza kuletwa ofisi ya WAWETA MAKAO MAKUU ofisi iko jirani
na ofisi ya idara ya Kilimo Halmashauri ya wilaya ya Tarime au ofisi ya idara ya
Kilimo kuanzia saa 1.30 hadi saa 9.30 alasiri siku zote mpaka tarehe ya mwisho
30/01/2017
Kwa mawasiliano simu namba: 0764218172, 0753193715
NB: MUOMBAJI ATAJIGHARAMIA USAFIRI NA FEDHA ZA KUJIKIMU
*MWISHO wa kutuma maombi haya ni tarehe 30/01/2017 saa 9.00 Alasiri, na
Usaili kwa wote waliotuma maombi utafanyika tarehe 31/01/2017 kuanzia saa
3.00 Asubuhi katika ofisi ya WAWETA iliyopo jirani na Ofisi ya kilimo ,
Halmashauri ya Wilaya Tarime.
Tembelea Job Site Tz kwa nafasi za kazi na ajira zaidi
Labels: NAFASI ZA KAZI