Aina Mpya za Mbegu za Mazao



Kamati ya Taifa ya Mbegu (National Seed Committee) imeidhinisha matumizi ya aina 29 za mbegu mpya za mazao mbali mbali ya kilimo. Mazao hayo ni mahindi, mpunga, alizeti, karanga na chai. Hatua hiyo ya Kamati inalenga kuongeza tija na kipato kwa mkulima.


Kuidhinishwa kwa aina hizo za mbegu kunafuatia mapendekezo yaliyofanywa na Kamati ya Taifa ya Kupitisha Aina Mpya za Mbegu za Mazao (The National Variety Release Committee) katika kikao chake kilichofanyika makao makuu ya Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Dar-es-saalam tarehe 16 na 17 Machi 2016.

Aina hizo mpya za mbegu zimepitishwa baada ya kufanyiwa utafiti na kugundulika kuwa zina sifa mbalimbali kama vile kutoa mavuno mengi, kustahimili ukame, ukinzani dhidi ya magonjwa na wadudu, kukomaa mapema na kupendwa na wakulima.

Kati ya aina hizo mpya za mbegu, kuna aina 16 za mahindi, 2 za mpunga, 4 za alizeti, karanga 3 na 4 za chai. Mbegu hizo zimefanyiwa utafiti wa kina na vituo vya utafiti vya Umma na sekta binafsi hapa nchini kama ifuatavyo:-

TAASISI/KAMPUNI
ZAO
AINA YA MBEGU
Kituo cha Utafiti Seliani
Mahindi
· SELIAN H215
Kituo cha Utafiti Naliendele                                       
Karanga                       
· NARINUT 2013
· NACHI 2013
· KUCHELE 2013
Kituo cha Utafiti Ilonga
Mahindi                      
  
                       
· WE4102
 · WE4106
· WE4110
· WE4114
· WE4115
Kituo cha Utafiti Tumbi
Mahindi
                   
· T104
· T105
Kituo cha Utafiti Chollima Dakawa                                   
Mpunga                              
· CH-SAT01
· CH-SAT09
Taasisi ya Utafiti wa Chai Tanzania                                    
Chai                   
                
· TRIT201/16
· TRIT201/43
· TRIT201/44
· TRIT201/55
Sunflower Development
Company (SDC)                              
Alizeti                                      
          
· NSFH36
· NSFH145
Advanta Seed Company Ltd
Alizeti
              
· AGUARA 4
· HYSUN 33
Meru Agro-Tours & Consultancy Co. Ltd                          
Mahindi                           
· MERU LISHE 503
· MERU LISHE 511
IFFA Seed Co Ltd
Mahindi
· KASPIDI HYBRID
· KISONGO HYBRID
Krishna Seed Co Ltd
Mahindi
· KRISHNA HYBRID-1
· KRISHNA HYBRID-2
Aminata Quality Seeds &
Consultancy Ltd                             
Mahindi                             
· NATA H 401
· NATA K8

Sifa za aina hizo mpya za mbegu zilizoidhinishwa na Kamati ya Taifa ya Mbegu
zimeambatanishwa katika Kiambatisho Na.1.
Aina hizo za mbegu zitaanza kuzalishwa na makampuni mbalimbali ya uzalishaji mbegu pamoja na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Kilimo (Agricultural Seed Agency - ASA). Lengo ni kuzifikisha aina hizo mpya za mbegu bora kwa wakulima kuanzia msimu wa 2017/2018.

Zaidi soma:
http://www.kilimo.go.tz/highlights/PRESS_RELAESE_FOR_2015_VARIETIES-MARCH_2016.pdf

Imetolewa na:
Mh. Mwigulu Mchemba
WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI

Labels: ,