Mambo Manne Unayotakiwa Kuyafanya Ili Kujua Thamani Ya Mazao Yako Na Kupanga Bei Yenye Faida

Mkulima ni mfanyabiashara, na mfanyabiashara yeyote ni mtu anayelenga faida kubwa au hasara kidogo. Kwa hiyo ni muhimu kwa mkulima kujua thamani ya mazao yake ili...

Habari za kazi ndugu yangu na karibu tena katika muendelezo wa makala zetu za kilimo cha kisasa. Leo nimeona nikufahamishe namna sahihi unayotakiwa kuitumia kujua thamani ya mazao yako na hivyo uweze kupanga bei isiyo na hasara kwako. Mkulima ni mfanyabiashara, na mfanyabiashara yeyote ni mtu anayelenga faida kubwa au hasara kidogo. Kwa hiyo ni muhimu kwa mkulima kujua thamani ya mazao yake ili aweze kujua ni bei gani anayotakiwa kuuzia mazao yake lakini pia ajue bei ambayo akiuza kwayo atapata hasara.

Mkulima-ni-mfanyabiashara

Nimeamua kuleta somo hili kwa sababu wakulima wengi wanauza mazao yao sio kwa sababu wameiona faida ila tu kwa sababu ya msukumo wa soko/madalali na bei iliyopo wakati husika. Hivyo basi natarajia mpaka mwisho wa somo hili utakuwa umejifunza mambo unayotakiwa kufanya ili ujue thamani ya mazao yako na uweze kujipangia bei yako mwenyewe yenye kukuletea faida bila ya kushawishiwa na madalali.

Kabla hutujaendelea: hapa chini nimekuchagulia baadhi ya makala za kilimo bora ni nzuri sana, bofya ili uzisome:

Okay tuendelee, sasa basi unachotakiwa kufanya ni:

HATUA YA KWANZA
Mali bila daftari hupotea bila habari”. Waliona mbali sana waliosema maneno haya. Mkulima unatakiwa uwe na daftari la kutunzia kumbukumbu za shughuri zako zote za shamba. Tunza kumbukumbu za gharama zote ulizozitumia katika kilimo chako. Kama ulikodi shamba au ulinunua, ulilima kwa trekta, ukaajiri watu wa kupanda, ukanunua mbolea na madawa ya kuulia magugu na wadudu, kama uliajiri watu wa kupiga dawa shambani, mpaka kuvuna n.k gharama zote ulizotumia katika shughuri hizi zihifadhi kwani hii ndio dira yako. Hakikisha kuwa unatambua ukubwa/eneo la shamba ulilolima kama ni hekta moja au mbili ama ni ekari tatu au nne. Hapa utapata jumla ya gharama ulizotumia katika uzalishaji kwa eneo husika.

HATUA YA PILI
Pima jumla ya kiasi cha mavuno yako. Kiasi cha mavuno unaweza kukipima kwa idadi ya magunia au matunda, kwa uzito (Kg) au ujazo (lita au debe). Napendekeza upime kwa magunia, kilo au/na idadi ya matunda kwa sababu ndio vipimo tunavyotumia kuuza bidhaa zetu sokoni. Kama ni vitunguu utapima kwa kilo au magunia, yaani ujue umevuna magunia mangapi katika eneo ulilolima. Kama ni matikiti/matango basi utapima kwa idadi ya matunda, yaani jumla ya matunda uliyovuna. Kama ni mchele basi utaupima kwa kilo ili ufahamu umepata jumla ya kilogram ngapi. Pima mavuno yako kwa njia yoyote unayoitumia wewe ilimradi tu mwisho wa siku ujue umevuna kiasi gani. Hapa utapata jumla ya mavuno kwa eneo husika.

HATUA YA TATU
Katika hatua hii gawanya jumla ya gharama za uzalishaji kwa kiasi cha mavuno. Lengo letu hapa ni kujua umegharamia pesa kiasi gani kwa gunia moja au kilo moja au kwa tunda moja ulilovuna. Hii ndiyo thamani ya mazao yako. Ili tuelewane vizuri hapa tuchukulie kwa mfano gharama za uzalishaji ni TSh. Milion moja na nusu ulizotumia katika ekari moja:

Sasa tupandishe kidogo gharama za uzalishaji, kutoka milioni moja na nusu mpaka milioni tatu kwa eneo lile lile la ekari moja:
Unajua ni kwanini tumebadilisha gharama za uzalishaji? Lengo letu hapa ni kuonesha jinsi gani gharama za uzalishaji zinavyochangia katika thamani ya mazao yako na hivyo katika kufanya maamuzi ya bei yako ya faida. Ikiwa gharama za uzalishaji ni kubwa basi mazao yako yanathamani kubwa na hivyo basi ili upate faida ni lazima uuze kwa bei kubwa kuliko thamani yake kama tutakavyoona hapa chini.

HATUA YA NNE:
Sasa baada ya kujua thamani ya gunia moja au kilo moja au tunda moja, hatua nyingine ambayo ndio muhimu zaidi ni kupanga bei sahihi yenye faida utakayouzia mazao yako. Hapa tunahitaji kupanga bei ya mazao kwa kipimo husika yaani bei ya gunia moja au kilo moja au tunda moja. Bei yenye faida kwako ni ile itakayorudisha gharama zote ulizotumia katika uzalishaji wako. Sasa rejea hatua ya tatu hapo juu:
Baada ya kujipangia bei yako sasa toka nje uangalie soko likoje, je bei uliyojipangia ni ndogo au kubwa kuliko iliyoko sokoni? Ikiwa bei uliyopanga kuuza mazao yako ni ndogo kuliko inayotembea sokoni kwa wakati huo (au bei ya sokoni ni nzuri zaidi kuliko uliyotegemea wewe) basi fanya hima uuze kwani utakuwa umevuka matarajio yako katika uzalishaji kitu ambacho kila mtu anakitamani.

Lakini ukiona bei ya sokoni ni mbaya yaani ni ndogo kuliko ile uliyotaka kuuzia mazao yako fanya moja kati ya yafuatayo:

Ushauri: katika kilimo chochote utakacho kifanya jitahidi sana kupunguza gharama za uzalishaji ili ujiongezee nafasi ya kupata faida kubwa zaidi. Punguza gharama zote zisizo za lazima, lakini usijisahau kiasi cha kuathiri ubora na wingi wa mavuno.

Kabla hatujamaliza kabisa nikukumbushe kuwa tumeshaandika baadhi ya makala za jinsi ya kufanya kilimo bora na chakisasa, zipo hapa chini (bofya kuzisoma):

Hivi ndivyo tunamaliza somo letu la leo, je umejifunza kitu chochote? Ulikuwa unafanyaje unapotaka kujua thamani ya mazao yako? Weka mawazo yako hapa chini kwenye comments. Tukutane tena Jumatatu ijayo katika makala nyingine tena...

Labels: